MBOZI. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Kasim Majaliwa Majaliwa amewaagiza mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kuhakikisha wanasimamia upangaji wa mji wa kibiashara wa Mlowo.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo Jumanne Februari 14, 2023 wakati wa ziara yake mkoani Songwe wakati akiongea na wananchi wa Mlowo wilayani Mbozi.
"Mji huu uanze kupangiliwa kwa kuwa ni mji unaokua kwa kasi kibiashara hivyo mwenyekiti na mkurugenzi muupange mji huu vizuri" ameagiza
Pia, Waziri Mkuu huyo ambaye leo ni siku ya pili ya ziara yake amewataka Tarura katika mkoa huo kuhakikisha barabara za mitaa zinakengwa kwa kiwango cha lami.
"Wananch wa Mlowo naomba mtambue kama huu ni mji wa kibiashara hivyo mjipange kwa kuwa na mji wa Vwawa wataanza nao kupambana wawafikie lakini msirudi nyuma nyie ndio mji wa kibiashara" amesema