• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

Kurushwa hewani: March 19th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamadi Mbega, amefanya ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika Kata ya Ipunga huku akihamasisha ushirikiano baina ya Serikali na jamii katika kutekeleza miradi ya maendeleo.


Katika ziara hiyo, Mhe. Mbega alitembelea Shule ya Msingi Ipunga na kujionea hali ya miundombinu ya shule pamoja na changamoto zinazowakumba walimu na wanafunzi huku akiwasisitiza walimu kuendelea kutoa elimu bora.


Pia, alitembelea Zahanati ya Kata ya Ipunga, ambapo alikagua utoaji wa huduma za afya kwa wananchi akisisitiza umuhimu wa kuboresha huduma hizo.


 DC Mbega ambaye alishiriki mkutano mkuu wa wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Kata ya Ipunga aliwataka wajumbe hao  kushirikiana kwa karibu na serikali katika kutatua changamoto za kijamii na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi na uzalendo mkubwa.


Aidha, amewahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii katika shughuli zao mbalimbali za kiuchumi kama kilimo, ufugaji, na biashara.


Katika ziara hiyo, Mhe. Mbega aliwasisitiza wananchi kuyasemea mazuri yanayofanywa na Serikali, ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama barabara, huduma za afya, na elimu. Alisisitiza kuwa ushirikiano kati ya serikali na wananchi ni msingi wa maendeleo endelevu.


Mhe. Mbega aliwaeleza wananchi umuhimu wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu pamoja na kutoa rai kwa wananchi kudumisha mshikamano na amani katika jamii, akieleza kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila ushirikiano wa kijamii na utulivu.


Ametoa wito kwa viongozi wa vijiji na kata kuhakikisha wanashirikiana na wananchi kuibua miradi mipya ya maendeleo na kuhakikisha rasilimali za umma zinatumiwa kwa manufaa ya jamii yote akieleza kuwa Serikali ya Wilaya itaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo kwa uadilifu na kuhakikisha changamoto zao zinashughulikiwa kwa wakati.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa