Wazazi wa wanafunzi wanaosoma shule ya Msingi Itete Kata ya Mlowo wamemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega madawati 140 yenye thamani ya zaidi ya Sh6 milioni ikiwa ni juhudi zao kutatua changamoto ya uhaba wa madawati katika shule hiyo.
Wazazi hao wamekabidhi madawati hayo leo Jumatatu Februari 17, 2024 wakati wa hafla iliyofanyika katika Shule ya Itete Kata ya Mlowo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Mbega amewashukuru wazazi hao kwa jitihadi hizo za kuamua kuchangia madawati ili kuwatatulia changamoto ya uhaba wa madawati.
"Niwashukuru sana wananchi kupitia wazazi hawa kwa kuonesha ubunifu wa kutatua changamoto kwa wanafunzi. hii inaonyesha kuwa mmeona kazi nzuri alizofanya Rais wetu Mheshimiwa, Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuwekeza katika sekta ya elimu. Mmeonyesha mfano wa kuigwa nawashauri wazazi wengine muige kwa wazazi hawa" amesema DC Mbega
Mhe. Mbega pia amewapa wazazi hao salamu na pongezi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Daniel Chongolo kwa jitihada hizo walizozionyesha.
Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya huyo, Mwakilishi wa wazazi hao amesema kuwa wazo la kutengeneza madawati hayo lilianza Januari 28, 2025 baada ya uongozi wa shule kuitisha mkutano na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo changamoto ya madawati ambapo wazazi waliazimia kuchangia ili kutengeneza madawati hayo.
Pia, wazazi hao wamechangia fedha kwaajili ya kuweka sakafu madarasa manne ili kuweka mazingira bora kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa