Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Esther Mahawe ameahidi kulivalia njuga suala la baadhi ya wahudumu wa afya wilayani humo wanaodaiwa kuwatoza fedha wanawake wajawazito na wanaotoa lugha zisizo na staha kwa wanawake hao wakati wanapokwenda kujifungua.
Mhe. Mahawe amesema hayo wakati wa mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Dkt. Francis Michael wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika mji Mdogo wa Mlowo.
Ametoa ahadi hiyo baada ya baadhi ya wananchi katika mji huo kulalamika kuwepo kwa kutozwa fedha wakiwapeleka ndugu zao kujifungua katika baadhi ya maeneo yakutolea huduma za afya.
Baada ya malalamiko hayo, Mkuu wa Wilaya huyo aliahidi namna kuyafanyia kazi malamamiko hayo na kuwachukulia hatua watumishi watakaobainika kufanya vitendo hivyo.
Amesema kuwa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu inaleta fedha nyingi ili kuboresha miundombinu na huduma za afya, wanaofanya hivyo wanarudisha nyuma juhudu za Rais Samia
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa