Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imepandisha bajeti yake ya mapato ya ndani kutoka bilioni 4.5 ya mwaka wa fedha 2024/24 kufikia bilioni 6.7 mwaka wa fedha 2024/25 ikiwa na ongezeko la asilimia 49.
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. George Musyani amesemakuwa ongezeko hilo linatokana na usimamizi mazubuti wa vyanzo vya mapato unaofanywa na ofisi ya mkuu wa Wilaya, waheshimiwa madiwani kwa kushirikiana na wataalamu
"Bajeti yetu inazidi kupanda kutokana na usimamizi madhubuti wa mapato unaofanywa na uongozi wa Wilaya kwa kushirikiana na wataalamu wa Halmashauri yetu"
"Leo katika Baraza la Madiwani tumefanya mapitio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23 na 2023/24 na pia tumefanya mapitio ya utekelezaji wa makisio ya bajeti tanayokwenda kukusanya 2024/25 uangalia maeneo tutakayoweza kufanya vizuri" ameeleza
"Hivyo katika baraza tulijikita katika kuhakikisha kuwa Yale maeneo ambayo hatukuweza kufanya vizuri kuweka mikakati itakayowezesha kufikia lengo ya hii bajeti mpya"
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa