Halmashauri yaWilaya ya Mbozi imefanya kikao cha tathmini ya matokeo ya darasa la saba na darasa la nne ili kupanga mikakati ya kuzidi kupandisha ufaulu wa madarasa hayo.
Kikao hicho kimefanyika leo Jumamosi Februari 10, 2024 katika ukumbi wa shule ya Sekondari ya Vwawa.
Akizungumza katika kikao hicho, Afisa Elimu Mkoa wa Songwe Mwl. Michael Leghola ameupongeza uongozi wa Halmashauri hiyo kwa kuitisha kikao hicho ambacho kiliambatana na utoaji wa motisha kwa walimu wakuu ambao shule zao zimefanya vizuri.
Amesema kuwa kwa kuwapa motisha walimu hao kunawafanya hata wengine ambao hawajapata kufanya vizuri ili wasiachwe nyuma
Pia amewapongeza walimu hao kwa usimamizi nzuri wa miradi ya elimu katika shule zao na kusema kuwa walimu hao wamekuwa mfano mziri wa kuigwa.
"Tumefanya ziara maeneo mengi kutembelea na kukagua miradi ya elimu, Mbozi mmefanya vizuri kuliko wengine" amesema
Kwa upande wake Afisa Elimu Msingi Mwl. Dorothy Mwandila amesema kuwa wameweka mikakati mbalimbali ambayo itasaidia kupandisha ufaulu kwa wanafunzi ikiwa ni pamoja na kutoa maswali 10 Kila Siku katika madarasa ya mitihani, kufanya ziara za mafunzo, kurekebisha ikama ya walimu, kufanya mitihani minne ya upimaji kiwilaya na kufanya ziara za ufuatiliaji
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa