MBOZI. Naibu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuaia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Songwe, Mohamed Shariff ametoa wito kwa wote wenye dhamana ya kutekeleza, kufuatilia na kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali mkoani humo kuhakikisha inatekelezwa kwa weledi na kwa wakati.
Shariff ametoa wito huo leo Jumanne 21 Februari 2023 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za Takukuru mkoa wa Songwe.
Amesema kuwa katika kufanya uchunguzi wa masuala mbalimbali yanayohusu rushwa Ofisi za Serikali za Mitaa ndio zinalalamikiwa zaidi ikifiatia elimu, polisi na kilimo.
Shariff ametaja sababu ya sekta ya Serikali za Mitaa kulalamikiwa zaidi ni kutokana na sekta hiyo kukutana na wananchi moja kwa moja ambapo kunakuwa na usumbufu, kutokuwepo maeneo ya kazi pamoja akutopokea simu.
"Serikali za Mitaa wanadeal na watu moja kwa moja endapo wasipotimiza wajibu wao ndio maana malalamiko yanakiwa mengi zaidi" amesema
"Niwaombe wanahabari kuendelea kuelimisha na kuuhabarisha umma ili jamii izidi kutambua wajibu wao katika kufichua vitendo viovu vyenye viashiria vya rushwa katika zoezi hili muhimu Kwa ustawi wa jamii" amesisitiza
Ametaja mkakati wa kwanza wa Taasisi hiyo wa kutokomeza rushwa kuwa ni kutoa elimu kupitia Takukuru _Rafiki ambayo itaongeza wigo wa kushirikisha wananchi na wadau katika kutambua na kutatua kero katika utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo zinazoweza kuisababisha kutolea vitendo vya rushwa.
Pia, Shariff amebainisha kuwa Takukuru imejipanga kufanya uchambuzi wa mfumo wa usimamizi wa mageti ya maliasili, mfumo wa usambazaji mbolea za ruzuku, kufanya ufuatiliaji wa fedha za mapato ya ndani ya halmashauri zinazopelekwa kwenye miradi, na asilimia 10.
Ameeleza kuwa kuwa katika kipindi cha robo ya pili taasisi hiyo imefanya ufuatiliaji wa miradi 68 yenye thamani ya Sh11.5 bilioni inayotekelezwa katika sekta ya afya, elimu, miundombinu, maji na mifugo
Ameongeza kuwa miradi iliyobainika kuwa na mapungufu hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na wahusika kuelekezwa kufanya marekebisho, kuongeza ufuatiliaji, kutunza vizuri nyaraka, kuongeza kasi ya ujenzi, kuwashauri wakurugenzi kuangalia namna ya kumalizia miradi kupitia vikao vya maamuzi.
Katika uchambuzi wa mfumo wa masoko taasisi hiyo imeshauri asilimia 20 ya mapato yanayokusanywa yarejeshwe ili masoko yaweze kujiendesha.
Pia, amesema Takukuru imeshauri halmashauri iteue au kuajiri maofisa masoko au mameneja ili waweze kusimamia uendeshaji wa masoko kama vile usafi, ulinzi, pamoja na uboreshaji wa moundombinu ya masoko hayo.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa