Ili kuendeleza elimu ya mapambano ya rushwa, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Songwe, imekabidhi zawadi kwa wanafunzi walioibuka kidedea katika uandishi wa insha katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi.
Zawadi hizo kwa washindi hao zimetolewa leo Alhamisi Januari 25, 2024 katika shule ya Sekondari Kisimani iliyoko Kata ya Mlowo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Dawati la kuzuia ruswa TAKUKURU,
Boniface Mwampashe amesemakuwa mashindano hayo ya uandishi wa insha yalihusiana na kuzuia rushwa katika jamii ambapo mada ilikuwa ni faida za kuzuia na kupambana na rushwa kwenye jamii na taifa kwa ujumla.
"Nafahamu wengi mnajua majukumu ya TAKUKURU lakini jukumu mojawapo ni kutoa elimu kwa umma kwa njia mbalimbali ikiwemo uandishi wa insha kwa wanafunzi ambapo wanafunzi wanapewa mada ya kujua wanafunzi Wana uelewa gani juu ya rushwa" amesema na kuongeza;
"Katika shindano hili shule 32 zilishirokinna wanafunzi 111 walishiriki kuandika insha na wanafunzi 3 wameibuka na ushindi ambao ni Emmanuel Origa kutoka Shule ya sekondari Kisimani, wapili Justine Ndambo sekondari ya Ihanda ambapo walipata alama sawa na Silivia Ilomo toka Sekondari ya Canan.
Mmoja wa washindi katika shindano hilo Emmanuel Origa ameishukuru TAKUKURU kwa kuanzisha vilabu vya kupinga rushwa mashuleni ambavyo vinasaidia wanafunzi kupata elimu juu ya masuala ya rushwa
"Tunaishukuru TAKUKURU kwa kuanzisha vilabu vya kupinga rushwa mashuleni tunapata elimu juu ya rushwa tunaahidi kuwa mfano bora katika jamii kutokana na elimu tulioipata kutoka katika vilabu hivi"
Kwa upande wake mwalimu wa shule ya Ihanda Ililo ambaye ni mlezi wa klabu ya wapinga rushwa katika shule hiyo amesema kuwa "Nimefurahi kwamba kupinga rushwa ni sehemu ya maisha yenu ninaimani mmeshatambua rushwa ni nini mnafahamu aina zake na madhara kwenu na kwa jamii,
Kila mmoja akafikishe elimu hii huko alikotoka kwa wazazi na kwawatu wanaowazunguka Ili wote wahusike na vita dhidi ya rushwa" amesisitiza
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa