• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

SIJAWAHI KUJUTIA KUFANYA KAZI MKOA WA SONGWE

Kurushwa hewani: March 21st, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba amesema kuwa hajutii kufanya kazi katika mkoa wa Songwe kutokana na ushirikiano alioupata kutaka kwa watumishi wa umma na wananchi wakati akiwa mkuu wa mkoa huo huku akiahidi kuwa Songwe itaendelea kubaki moyoni mwake.


Kindamba alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe akihamishiwa mkoa wa Tanga na Rais Samia Suluhu Hassan Februari 26 mwaka huu ambapo nafasi yake ikichukuliwa na Dkt Francis Michael.


Akizungumza wakati wa kukabidhiana ofisi na mkuu wa mkoa huo mpya leo Jumatatu Machi 20, 2023 Kindamba amesema wafanyakazi wengi katika mkoa huo waliishi naye kama ndugu hivyo Songwe itaendelea kubaki moyoni mwake.


"Hamkuwa wafanyakazi tu ila mlikuwa ndugu zangu, mara nyingi familia yangu ilikuwa Dar es Salaam lakini ninyi mlikuwa kama ndugu zangu, kutokana na ushirikiano mliokuwa mnanipa. Sijawahi kujutia kufanya kazi Songwe na itaendelea kubaki moyoni mwangu" amewaambia viongozi na watumishi wa mkoa huo wakati akikabidhi ofisi.


Amebainisha kuwa uahirikiano alioupata ndio uliowezesha kutatua mogogoro ya mara kwa mara katika mji wa Tunduma.


"Tunduma ilikuwa inachemka na migogoro lakini tuliweza kushirikishana na kwa ushirikiano mambo yakawa shwari. Tunduma imepoa kwa sababu ya kushirikishana kutatua migogoro" amesema Kindamba na kuongeza


"Nawashukuru viongozi wenzangu kuanzia ngazi ya mkoa hadi vijiji, tulifanikiwa kwa sababu tulifanya kazi kama timu"


Pia, Kindamba amewataka viongozi na wananchi wa mkoa wa Songwe kupinga ukatili wa kijinsia na vitendo vingine vinavyokwenda kinyume na maadili.


Hata hivyo, Kindamba amemshauri mkuu wa mkoa huyo kuendeleza vipaumbele vilivyokuwa vimewekwa ikiwemo ujenzi wa Bandari Kavu eneo la Mpemba, upanuzi wa barabara ya TANZAM iwe njia nne, mji wa kisasa kata ya Mpemba, stendi ya kisasa ya mkoa na utatuzi wa migogoro ya mipaka.


Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Songwe (RAS), Happiness Seneda amemshukuru Kindamba kwa namna alivyoishi vizuri na watumishi wa umma wa mkoa huo na kubainisha kuwa Mkuu huyo wa mkoa wa Tanga alikuwa mwalimu kwa wengi wakati akiwa katika mkoa huo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa