Afisa mradi wa Shirika la SAWA, Bi. Rebeca Magurusa amesema kuwa moja ya mikakati ya mradi wa SHH kutoka Shirika hilo ni kuhakikisha wanatoa elimu kuhusiana na masuala ya hedhi salama kwa vijana ambao wapo nje ya shule, ndani ya shule na jamii inayowazunguka ili kuwa na uelewa juu ya suala hilo.
Mratibu huyo ameyasema hayo leo Jumanne Januari 23, 2024 wakati wa kikao cha kutambulisha mradi huo unaofadhiliwa na Shirika la Watoto Duniani (Unicef).
Rebeca ameitaja mikoa itakayotekeleza mradi huo kuwa ni Mbeya na Songwe katika wilaya nne ambazo ni Mbozi, Momba, Mbeya na Mbalali.
Ameongeza kuwa katika wilaya ya Mbozi mradi huo utafanyika katika shule 15 za msingi na mbili za sekondari, pamoja na jamii inayozunguka maeneo ya shule hizo kupitia mradi huo uliojikita katika kutoa elimu ya masuala ya hedhi salama.
Amesema kuwa kuna vikundi ambavyo vimeundwa na kujengewa uwezo wa kufanya shughuli mbalimbali za ujasiliamali ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa taulo za kike zinazofuliwa na kutumiwa tena.
‘’Kwa Wilaya ya Mbozi tayari tuna vikundi vine ambavyo vinatengeneza bidhaa mbalimbali pamoja na kuuza taulo hizo ambazo zinauzwa kwa jamii ili kuzitumia kwa wakati wa hedhi’’ amesema Magurusa.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa