Songwe. Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Waziri Kindamba ametoa wito kwa washitiri walioingia mkataba na mkoa huo kuwa wanahakikisha wanasambaza kwa wakati mahitaji yanayotakiwa kusambazwa katika halmashauri huku wakizingatia ubora na thamami ya dawa.
RC Kindamba ametoa wito huo leo Jumanne Januari 7, 2023 wakati wa hafla ya kusaini mikataba ya washitiri watakaosambaza dawa na vifaa tiba katika mkoa huo.
Mkuu wa mkoa huyo amesema kuwa katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2023, mkoa umepokea dawa na bidhaa nyingine za afya zenye thamani ya shilingi bilioni 2.2 kutokana na fedha za ruzuku ya Serikali kupitia Bohari ya Dawa (MSD) pamoja na mapokezi ya vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.3.
Pia, RC Kindamba amebainisha kuwa katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2023 Serikali imetoa jumla ya shilingi 1.6 kwaajili ya ununuzi wa vifaa tiba muhimu kwa lengo la kuhakikisha miundombinu ya kutolea huduna za afya na zahanati mara itakapokamilika ianze kutoa huduma zinazokusudiwa
Ameongeza kuwa kwa mujibu wa mwongozo huo mkoa unatakiwa kuwa na washitiri wanne au pungufu.
Ameeleza kuwa kutokana na taratibu, mkoa umekamilisha mchakato wa kupata washitiri wawili ambao ni Astra Pharm (T) Ltd ambaye atahusika kusambaza dawa na vifaa tiba, na mwingine Anudha Ltd ambaye atahusika na kusambaza vifaa vya maabara na mifupa.
Amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote kusimamia mapokezi ya vifaa hivyo kutoka kwa washitiri na kuongeza kuwa katika suala za usimamizi watanzania wengi hatuwi makini.
"Mama Samia anahangaika analeta fedha nyingi ili huduma bora ziwafikie wananchi wake naomba tukalisimamie hili" amesema
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa