Songwe.Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Waziri Kindamba amewataka wananchi wa mkoa huo kutumia elimu waliyoipata wakati wa maadhimisho ya wiki ya Sheria iwasaidie kupata suluhu ya migogoro katika jamii huku akiwaasa kutoka zama za kuuza ng'ombe kwa kesi ya kuku.
RC Kindamba ametoa rai hiyo leo Jumatano Februari mosi, 2023 wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya Sheria ambayo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Songwe iliopo Nselewa.
Tutoke katika enzi za kuuza ng'ombe Kwa kesi ya kuku, lazima tutafute Suluhu ya migogoro yetu
Amesema kuwa kupitia maadhimisho hayo wadau wa mahakama watawaongoza wadaawa ambao ni mshtaki na mshtakiwa katika kutatua mgogoro wao kwa njia ya usuluhishi.
"Ni matumaini yangu watu wa mahakama na wananchi wa Mkoa wa Songwe wameyatendea haki maadhimisho ya wiki ya Sheria mpaka kufikia leo kilelele cha maadhimisho hayo kwa kujitokeza kupata elimu na kufahamu hatua mbalimbali za kufungua majalada mahakamani" amesema mkuu huyo wa mkoa.
Katika maadhimisho hayo yenye kaulimbiu umuhimu wa kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi endelevu: wajibu wa mahakama, RC Kindamba ametoa wito kwa jamii kutafuta njia bora za utatuzi wa migogoro na si kuendeleza zilizopitwa na wakati.
"Tutoke katika enzi za kuuza ng'ombe kwa kesi ya kuku, lazima tutafute suluhu ya migogoro yetu" amesesitiza mkuu huyo wa mkoa na kuongeza;
"Mkoa wetu sio kisiwa tumeshuhudia mama Samia (Rais Samia Suluhu Hassan) ameruhusu mikutano ya kidemokrasia kutafuta suluhu ya migongano mbalimbali ili kulinda haki na usawa katika jamii" amesema
Ameeleza kuwa Rais Samia anatamani watanzania wote wanapata haki maana haki ni msumeno inakata mbele na nyuma hata vitabu vya dini vimeandika.
"Mahakama imekuja na hili kwani suluhu huleta mahusiano mazuri kuliko kupekekana mahakamani kumaliza muda, pesa husababisha kutopata mahusiano mazuri" amesema
Amewataka waliopewa zamana ya kuwasimamia wananchi watende haki.
Akisoma hotuba yake kwa mgeni rasmi Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Hassan Makube amesema kuwa mahakama inajukumu la kuhakikisha kuwa suala la utoaji haki linafanyika kwa wakati ili kuwezesha wananchi kufanya shughuli zao za kimaendeleo
Amezitaja faida za kutatua migogoro kuwa ni pamoja na upatikanaji wa haki kwa wakati kwani hakutakuwa na matumizi mengi ya taratibu za kisheria
"Pia hupunguza mlundikano wa mashauri mahakamani, watu watapata muda mwingi wa kufanya shughuli za maendeleo" amesema
"Vilevile itasaidia kuimarisha amani na ustawi wa jamii kwasababu italinda uhusiana wa wadaawa hasa pale kunapokuwa na mgogoro" ameeleza Makube
Makube amezitaja changamoto za kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi kuwa ni uelewa mdogo wa njia hii, kutokuwa tayari kujishihusha na gharama ya kuwalipa wasuluhishi nje ya mahakama.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Momba, Fakii Lulandala ambaye amekaimu nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Esther Mahawe amesema kuwa katika moja ya jukumu la ofisi ya mkuu wa wilaya ni usuluhishi wa migogoro hivyo ofisi hiyo ninapunguza kesi mahakamani
"Sisi ni miongoni mwa wahusika tunatamani kuona mahakama inafanya kazi kwa ufanisi na maridhiano" ameswma DC huyo
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa