SONGWE. Mkuu wa Mkoa wa Songwe (RC), Waziri Waziri Kindamba ameahidi kuwa ofisi yake itatoa ushirikiano kwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga katika mkoa huo kwani wao ndio injini ya uchumi katika jamii.
RC Kindamba ametoa ahadi hiyo wakati akikabidhi hati ya kiwanja ambacho kitajengwa ofisi za wafanyabiashara hao.
Wafanyabiashara hao wamekabidhia hati ya kiwanja hicho ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa Serikali wa kuwajengea miundomninu na mazingira rafiki wafanyabiashara hao baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutoa Sh10 milioni kwa kila mkoa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za machinga.
Akikabidhi hati hiyo, RC akindamba amesema " Mheshimiwa Rais Samia ameamua kutenga Sh10 milioni kila mkoa ili kuwajengea wamachinga ofisi kwasababu ni mamilionea wajao,
"Ofisi yenu itakuwa hapa jirani na ofisi ya mkuu wa mkoa ili iwe rahisi kuja kupewa msaada mtakapokua mmekwama" amesema mkuu huyo wa mkoa.
"Sisi kama mkoa tutaongeza nguvu katika kiasi hicho mlichotengewa na mama ili ofisi iwe ya kisasa zaidi" ameahidi RC Kindamba na kuongeza;
Sisi kama mkoa tumejipanga kuwa bega kwa bega na ninyi kwani hata mbuyu ulianza kama mchicha".
Ameeleza kuwa kazi ya Serikali kuwawekea mazingira mazuri wamachinga hao ili kuepusha migogoro na kuwangunisha na huduma za kibenki.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe (RAS), Happiness Seneda amewapongeza wamachinga kwa kupewa hati hiyo huku akiahidi usimamizi wa ujenzi wa ofisi hiyo.
Katibu tawala huyo amebainisha kuwa "Hati hii iliyo na miaka 99 ni hati iliyoandikwa Mbozi kwakuwa ndio makao makuu ya mkoa".
Akizungumza baada ha kukabidhiwa hati hiyo kwa niaba ya wafanyabiashara hayo, mwenyekiti wa Umoja wa Wamachinga Mkoa wa Songwe, Kelvin Kyando amemshukuru Rais Samia kwa kuendelea kuwajali na kuahidi kulipa fadhila 2025.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa