• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

RAS SENEDA AWATAKA WAUGUZI KUTOA HUDUMA BORA BILA UBAGUZI, AKIONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAUGUZI SONGWE

Kurushwa hewani: May 31st, 2024

Wauguzi wa Mkoa wa Songwe wametakiwa  kuendelea kutoa huduma bora na salama kwa kuheshimu utu wa mtu bila ubaguzi.


Wito huo umetolewa na leo Ijumaa Mei 31, 2024 na Katibu Tawala Mkoa wa Songwe Bi.  Happiness Seneda wakati wa kilele cha  Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani ambapo kimkoa yamefanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi.


Akizungumza katika maadhimisho hayo, Bi. Seneda amesema kuwa jamii inatambua kazi kubwa inayofanywa na wauguzi.


"Ninafahamu kuwa wauguzi wengi wanafanya kazi zao vizuri kwa kuzingatia maadili na msingi bora ya taaluma yao, ingawa wapo wachache ambao wanataka kuichafua taaluma" amedokeza na kuongeza;


"Natoa wito kwa viongozi, wauguzi hao wanaokwenda kinyume na maadili ya taaluma yenu msiwafumbie macho, bali mfanye jitihada za kuwabaini na kuwarekebisha. Mamlaka zao za nidhamu ziwachukulie na hatua za kimaadili kwa kuwafikisha kwenye baraza lenu"


"Nimesikia changamoto mlizowasilisha ambazo kwa namna moja au nyingine zinachangia kupunguza ubora wa utendaji kazi zenu ikiwa ni pamoja na upungufu wa wauguzi katika vituo vya kutolea huduma, hili ni tatizo la nchi nzima pamoja na tatizo hili Rais wetu anaendelea kutoa ajira kwa awamu tofauti"


Kuhusu suala la waajiri kutowaruhusu wauguzi kushiriki makongamano ya kitaaluma kwa kushindwa kuwagharamia, Katibu Tawala huyo  amewaagiza wakurugenzi kutenga fungu la kuwawezesha wauguzi hao kushiriki.


Akizungumzia changamoto ya wauguzi kutopata posho ya sare ya kazi, amesema kuwa kuwa ni takwa la kimuundo hivyo ni wajibu wa waajiri wote kuhakikisha wauguzi wanapatiwa posho ya sare za kazi.


Siku ya Wauguzi duniani huadhimishwa  kwa heshima ya Wauguzi na wafanyakazi wa afya ulimwenguni kote.


Siku hii ilitengenezwa kwa heshima ya Florence Nightingale, ambaye alikuwa muuguzi maarufu uingereza na manzilishi wa taaluma ya uuguzi wa kisasa

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa