Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) kimetembelea maeneo ya miradi inayotarajiwa kutekelezwa katika Wilaya ya Mbozi huku kikitoa mafunzo ya uibuaji wa miradi inayoweza kutekelezwa kupitia ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPPC) kwa wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi.
Ziara hiyo imefanyika leo Jumatatu Februari 17, 2025 ambapo wakufunzi Dk Bravious Kahyoza na Christine Kaigarula kutoka PPPC walianza kwa kutoa mafunzo ya uibuaji wa miradi inayoweza kutekelezwa kupitia ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPP) kabla ya kutembelea maeneo ya miradi hiyo.
Mafunzo hayo yalielimisha umuhimu wa PPP na namna Halmashauri inavyoweza kunufaika kupitia ubia baina ya Serikali na Sekta Binafsi.
Maeneo ya Miradi waliyotembelea maafisa hao ni pamoja eneo la Mbozi klabu, soko la Ichenjezya, Stendi ya Malori na eneo la Generation
Kituo cha Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre) kimeanzisha mafunzo mikoa 12 kwa ajili ya kusaidia uibuaji wa miradi inayoweza kutekelezwa kwa mfumo wa ubia
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa