• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU WAZIRI KIGAHE ASEMA TANZANIA INAHITAJI VIWANDA VYA KUONGEZA THAMANI MAZAO YA KILIMO SONGWE

Kurushwa hewani: August 10th, 2023

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amesema Tanzania ina uhitaji wa viwanda vya kuongeza thamani mazao ya kilimo kwa kuwa zaidi ya asilimia 65 wamejiajiri katika kilimo.

Kigahe amebainisha hayo leo Jumatano Agosti 10, 2023 wakati wa ziara yake ya kutembelea Kiwanda cha Kahawa cha GDM na Kiwanda cha Ilasi Sembe katika Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe.

Amesema kuwa kama mazao yataongezewa thamani itakuwa tija kwa wakulima na mapato yataongezeka.

 "Viwanda hivi vinavyoongeza thamani mazao ya kilimo vitasaidia mazao yetu yaongezewe thamani ili kuleta tija na mapato kwa wakulima" ameeleza

Naibu Waziri huyo ambaye alikuwa anahitimisha ziara yake ya Siku mbili mkoani Songwe amesema changamoto inayozikumba nchi nyingi za Afrika ni kuzalisha bidhaa ambazo hawazitumii.

Ametoa wito kwa viwanda ambavyo vinategemea malighafi kutoka kwa wakulima kuwasaidia pembejeo na mbegu ili wazalishe kwa tija hali itakayosaidia viwanda kupata malighafi.

Hata hivyo, Kigahe ameipongeza Mkoa wa Songwe na Halmashauri ya Wilaya  ya Mbozi kwa usimamizi mzuri wa minada ya kahawa.

"Niwapongeze Mkoa na Halmashauri (Mbozi) kwa kuhakikisha minada ya kahawa inafanyika hapa Mbozi  zamani mlikuwa mnategemea kule Moshi na Arusha ambapo inakuwa gharama kusafirisha" amesema

Amesema kazi ya Wizara hiyo ni kuweka mazingira wezeshi ikiwa ni mojawapo ya mkakati wa kuboresha uwekezaji.

"Tumekubaliana kuanzisha eneo huru la biashara kama nchi za Afrika kuuziana sisi kama sisi. Tumeshaanza kufanyiana hivyo na sisi Tanzania tunapata fursa kubwa kuwauzia kwa bei nzuri" amesema

Naibu Waziri huyo amehitimisha ziara yake ya siku mbili mkoani Songwe ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea Kituo cha Pamoja cha Forodha Tunduma, kutembelea Kiwanda cha Kahawa cha GDM, Kiwanda cha Ilasi Sembe na kuhitimisha kwa kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa mkoa wa Songwe

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa