Mradi wa duka la mahitaji ya Nyumbani unaoendeshwa na Olida Mwamboneke mnufaika wa TASAF umekuwa tegemeo kwa wakazi wa kijiji cha Zelezeta katika kujipatia mahitaji mbalimbali ya Nyumbani.Mwamboneke amesema baada ya kupata pesa 32,000 ya TASAF aliamua kuanza kuuza mafuta ya kupikia kwa kuanza na ndoo ya lita 10 kisha kuuza kwa kupima ya shilingi 100 hadi sasa ananunua ndoo ya lita 20 ya mafuta.Kwa sasa nauza sabuni, sukari, nyanya, chumvi, soda na mahitaji mhimu ya Nyumbani kwa hapa kijijini yanapatikana dukani alieleza mnufaika wa TASAF, Mwamboneke."Kilichonivutia kuanza Biashara hii niliona baada ya kuchukua fedha za TASAF 32,000 mimi na majirani zangu tukawa tunatembea umbali wa mita 300 hadi 500 kufuata mahitaji madogo kama mafuta ya kula, sabuni na nyanya hali iliyopelekea mimi kuja na wazo la kuanza kuuza mahitaji ya Nyumbani.Mkazi wa kijiji cha Zelezeta na jirani wa mnufaika wa TASAF, Saimon Msukwa anamshukuru mnufaika kwa kuwafupishia muda wa kutembea umbali mrefu kufuata mahitaji na ametoa wito kwa wanufaika wengine ni vyema wawe na lengo la kuwekeza kwenye miradi ya kuwagusa jamii kama alivyofanya, Mwamboneke.Pamoja na kuwa na duka, mnufaika pia ameweza kulima mahindi ekari 1 kwa kutumia mbegu ya kisasa na anategemea kupata gunia zaidi ya 18, amelima maharagwe anategemea kupata debe 2 na amefuga Nguruwe wa 3.Bwn. Salim Bakari mlezi wa Kata ya Igamba kwa TASAF amesema kwa kijiji cha Zelezeta chenye wanufaika 67 na Mwamboneke amekuwa kielelezo kizuri kwa wanufaika wengine.Mtendaji wa kijiji cha Zelezeta, Tusajigwe Mwakyembe amesema wanufaika wa TASAF kuwa na uhakika wa milo 3 kwa siku wamekuwa chachu ya maendeleo kwenye kijiji na Serikali ya kijiji tumekuwa mstari wa mbele wa kuwapatia elimu juu ya matumizi sahihi ya fedha wanazopata ili yalenge malengo yanayokusudia ya kuwakwamua katika umasikini.Mwamboneke aliachana na mume wake na anaishi katika Nyumba ya Familia na ana watoto wa 2 ambao wanapata mahitaji ya Shule kupitia mafanikio ya TASAF aliyopata mama yao.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa