• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

MBOZI WATAKIWA KULINDA MIUNDOMBINU YA UMEME

Kurushwa hewani: August 5th, 2023

Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Umeme Vijijini, Mhandisi Hassan Said amewataka wananchi wa Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe kutunza na kulinda miundombinu ya umeme huku akiwataka kuhakikisha wanatumia umeme kwa usalama.

Mkurugenzi huyo ametoa rai hiyo leo Jumamosi Agosti 5, 2023 akiwa katika Kata ya Bara na Isansa  Wilayani Mbozi wakati wa ziara ya kuzindua mradi wa nishati mzunguko wa pili katika kata hizo.

Amesema "Rai yangu mtunze na kulinda miundombinu hii na mhakikishe kuwa matumizi ya umeme yanatumika salama hasa kwa vijana wadogo. Tuepuke kukaa chini ya transifoma" amesisitiza

Mkurugenzi huyo amewasisitiza wananchi ambao bado hawajaomba umeme waombe ili wawekewe nishati hiyo.

Amesema kuwa kuna mradi mpya ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni katika Mkoa wa Songwe ambapo vitongoji 151 vitasambaziwa umeme kati ya hivyo 68 kutoka Wilaya ya Mbozi sawa na asilimia 45 ya mradi huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Umeme Vijijini, Janeth Mbene amesema kuwa Serikali imeweka historia kupeleka umeme vijijini ikiwemo  katika kata ya Bara na Isansa Wilayani Mbozi ambayo ilikuwa haijapata umeme tangu uhuru.

"Kwa bahati nzuri fedha za kuendesha nishati vijijini zipo mama yetu (Rais Samia) anahakikisha kuwa hela haikomi kutokana na vyanzo mbalimbali ambavyo vipo serikalini. Lengo la kuleta umeme ni kuchochea uchumi" amesema

Naye Mkurugenzi wa Tanesco Kanda ya Kusini Magharibi, Mhandisi Sotko Nombo amewatahadharisha wananchi kutokufanya shughuli za kijamii chini ya laini kubwa ya kupitisha umeme.

Mhandisi Nombo amewataka wananchi wa kata hiyo kuomba kuunganishiwa umeme ambapo gharama yake ni Sh27, 000 kwa maeneo hayo ya vijijini.

Mbunge wa Mbozi, Ranwelo Mwanisongole amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza wajibu wake wa kuwapelekea wananchi umeme.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa