MBOZI. Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Songwe imefanya ziara kukagua miradi ya barabara inayotekelezwa na serikali katika mkoa huo.
Ziara hiyo imefanyika leo Ijumaa Februari 24, 2023 katika mji wa Mlowo wilayani Mbozi ikiwa ni ziara ya siku tatu katika mkoa huo.
Kamati hiyo ambayo imeongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe (RAS), Happiness Seneda imetembelea eneo lililopendekezwa na Wakala wa Barabara Tanroad mkoa wa Songwe kwaajili ya kujenga kituo cha kushusha abiria lengo la kituo hicho kitajengwa ilikupunguza adha wanayoipata abiria katika mji wa Mlowo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa aliyoyatoa hivi karibuni akiwa kwenye ziara katika mkoa huo.
Katika ziara hiyo, Katibu Tawala huyo wa Mkoa ametoa maagizo kuwa magari yote lazima yaingie kituo cha mabasi cha Mlowo.
Ziara hiyo ya siku tatu imelenga kukagua utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya barabara katika Mkoa wa Songwe ambayo inasimamiwa na Tanroads mkoa wa Songwe.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa