MBOZI. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Danny Tweve ameziagiza shule za msingi na sekondari ambazo hazijaanza kutoa chakula kwa wanafunzi katika wilaya hiyo kuanza mara moja kwa kuwa bila kufanya hivyo ni kukiuka maagizo ya Serikali.
Maelekezo hayo yametolewa jana Jumatano Februari 22, 2022 wakati wa kikao cha lishe ambapo idara na taasisi mbalimbali zilikuwa zikitoa taarifa za utekelezaji wa miakakati waliojiwekea katika kikao kilichopita.
Katika kikao hicho kaimu mkurugenzi huyo amesema kuwa idara ya elimu msingi na sekondari walipewa agizo la kuanzisha clabu za lishe mashuleni ili kuinua kiwango cha lishe mashuleni ili kutokomeza tatizo la udumavu.
"Kulikuwa na maelekezo shule zote za msingi na sekondari wanafunzi lazima wapewe chakula shuleni;
"Naamini hilo sio ombi ni Sheria inataka hivyo na zile Sheria ndogondogo zilizowekwa na vijiji zifuatwe ili kutokomeza suala la udumavu" amesisitiza
Ameongeza kuwa "Tuongeze usimamizi shirikishi kwa yale maeneo ambako hizi program za lishe zinatekelezwa" amesisitiza
Mwekahazina wa Halmashauri hiyo, Emmanuel Masele amesema kuwa "Katika kuhakikisha shule zote zinapata chakula tungepata mrejesho kutoka kwenye ngazi ya kijiji na kata ili kuleta taarifa ya lishe katika maeneo yao hasa mashuleni" amesema
Kwa upande wake afisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Zainab Mkundawantu amesema kuwa taarifa zipo na zinawasilishwa kwa maandishi.
"Katika kata na vijiji tunapokea taarifa hizi na tunazifanyia kazi" amesema
Naye kaimu afisa elimu msingi Amani Malima amesema wameshawaagiza walimu wakuu kwamba kila shule inatakiwa kulima bustani ya mbogamboga.
Mratibu wa mradi wa kibowavi Martha Mchaki kutoka Shirika la ADP Mbozi mradi uliofadhiliwa na umoja wa ulaya kupitia program ya Agri - connect unaotekelezwa kwa uhamasishaji wa lishe mashuleni na kusaidia upandaji miti ya matunda na bustani za mbogamboga amesema "Tunasaidia kaya zenye watoto wenye utapia mlo kwa kuwapatia mbegu za mbogamboga za majani na mbegu za matunda"
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa