MBOZI. Naibu waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amewataka viongozi wa hospitali ya mkoa wa Songwe na wilaya ya Mbozi kuboresha huduma za hospitali zao ili waweze kupata wateja wengi hata wanaokwenda hospitali binafsi kwa kukosa huduma bora.
Dk Mollel amesema hayo jana Jumatano Februari 15, 2023 wakati wa ziara ya Naibu waziri huyo akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ikiwa na maagizo ya Waziri Mkuu aliyepaswa kutembelea hospitali hiyo baada ya kupata dharura, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya ziara katika hospitali hizo.
Katika ziara hiyo Naibu waziri huyo amesema kuwa hajaja kuwahukumu lakini amekuja kuwakumbusha watumishi wa afya majukumu yao
‘’Hongereni kwa kufanya kazi vizuri sehemu nyingi wanajisahau kama wapo chini ya RMO, na Pia DC katika wilaya ndio mwenye wizara zote muelewe ukielewa utakaa vizuri na serikari’’ alipongeza
Hata hivyo hakikisheni ripoti za Hospitali zinafika kwa mkuu wa mkoa aweanajua nini kinaendelea msifanye vitu kimya kimya hakikisheni vitu vinakaa sawa RMO wasimamie vizuri iliwaweze kufanya kazi hii kwa uadirifu inatakiwa tubadilike jitahidini
Kama hospitali mpya, mkoa mpya nawapongeza kwa huduma nzuri na makusanyo mnapata hela nyingi kwa mwezi mfanye vizuri pia katika matumizi ya fedha.
Kwa upande wa kukamilisha ujenzi Naibu Waziri Mollel ametaka wakandarasi waliopewa kazi hiyo kumaliza kazi kwa wakati na endapo wanapewa kazi kwa sharti la kutoa marejesho kwa waliwapa kazi watoe taarifa
‘’ Kuna wakandarasi wengine wanashindwa kumaliza kazi kisa marejesho ndio maana kila siku miradi inapanda bei tuambieni’’
Ripoti nitakayo poleka niyale makaratasi mlio jikomiti malizieni kazi
Naibu waziri huyo amemwagiza mganga mkuu wa wilaya ya Mbozi kuwasimamia vizuri watu wake ambao ni Incharge, Katibu wa afya , Mhasibu, Mfamasia
Ameongeza kuwa akiondoka hapo anatamani kuona mabadiliko mazuri yanatokea na kusema kuwa sisi lengo letu mfanye vizuri ilimkuu wa wilaya, mkurugenzi na watumishi wote mtimize majukumu yenu bila matatizo yoyote.
Hata hivyo kwa upandewake mfamasia wa hosptiali hiyo Jeremiah Luka ameomba kwa Naibu Waziri wa afya kutanuliwa wigo wa bajeti ili waweze kuagiza dawa katika hospitali hiyo kutokana na hospitali hiyo ilikabidhiwa na mkoa bila kuwa na bajeti ya uendeshaji .
Hata hivyo mwekahazina wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi Emmanuel Masele amefafanua kuwa, kama alivyo eleza mfamasia wakati wanavyopokea hospitali hawakuwa na bajeti kitendo kilichopelekea kuomba saplimentari bajeti ndani ya bajeti ya user fee ambapo kiasi cha shilingi 187 milioni zilifanikiwa kupatikana wakati uhalisia wa makusanyo ni shilingi zaidi ya milioni 400 hivyo hospitali inakusanya bilakuwa na vifungu vya kufanya malipo ya dawa, kwa sasa tupo kwenye mchakato wa bajeti 2023-24 tumezingatia vifungu vya hospitali hii.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mbozi, Esther Mahawe amemshukuru na kumpongeza Naibu Waziri wa afya kwa kuwafungua macho na kusema kuwa tulipo ambiwa tunamapungufu tujirekebishe
‘’Sasa twendeni tukajipange kuna changamoto hata yale Malalamiko kwa ya wananchi kwa waziri mkuu inawezekana ni kweli inawezekana upo sahihi wewe sio mwizi lakini the way unavyo weka mambo yako unasababisha mashaka yasio ya lazima kwa hiyo kila mtu afanye kazi yake’’
Tuweze kuwahudumia wananchi inauma sana leo hii Rais akisikia wananchi wake hawapati dawa wakati kila siku fedha zinatolewa kwaajili ya dawa
‘’Mimi naomba sana kulingana na kile ambacho mmeelekezwa na Naibu Waziri twendeni tukakifanyie kazi’’ amesisitiza
Nakuagiza DMO mbele ya Naibu waziri uwe unaripoti kwenye kamati ya ulinzi na usalama kila tutakapo kuwa na kikao cha usalama utafahamishwa ili utuletee mapato na matumizi na changamoto zinazoikumba hospitali ya wilaya ili wote tuwe na uelewa wa pamoja.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa