Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega amezindua kampeni maalumu ya upandaji miti katika Wilaya ya Mbozi kwa mwaka 2025.
Uzinduzi huo kiwilaya umefanyika leo Jumamosi katika Shule ya Msingi Ifungo iliyopo katika mji mdogo wa Mlowo
Katika uzinduzi huo, zaidi ya miti 1500 imepandwa ikiwa ni kuashiria uzinduzi wa kampeni hiyo.
Akizungumza baada ya uzinduzi huo, Mhe Mbega amesema lengo la Taifa ni kila wilaya kupanda miti milioni 1.5 kwa mwaka na lengo la mkoa ni kupenda miti zaidi ya miilioni 2 ambapo Wilaya hiyo inatarajia kupanda zaidi ya miti milioni mbili kwa mwaka.
"Upandaji miti siku ya leo ni utekelezaji wa Maelekezo ya Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya utekelezaji wa hifadhi ya mazingira. Aidha Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 2020-2025 ibara ya 235 (a) imeelekeza kukabiliana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi ambapo kila Halmashauri inatakiwa kupanda miti isiyopungua milioni 1.5 kwa mwaka" amesema na kuongeza
"Halmashauri yetu kufikia Januari 2025 imefanikiwa kupanda jumla ya miti 56,433.
Nimejulishwa kuwa shule ya Msingi Ifungo ni moja wapo ya shule ambayo ipo kwenye eneo linalokumbwa na upepo mkali. Hali hii inafanya shule hii kuwa na hali hatarishi ya kukumbwa na janga la upepo ambalo linaweza kupelekea uharibifu wa miundombinu ya shule na kuathiri elimu, afya kwa watumishi na wanafunzi kwa ujumla" amesema
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa