Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Esther Mahawe amewataka wananchi wa Kata ya Ihanda Kijiji Cha Iboya Wilayani humo kuwa watulivu kusubiri ulipwaji wa fidia kupisha ujenzi wa Kituo cha Ukaguzi wa pamoja
Mhe. Mahawe amesema hayo leo Alhamisi Februari 15, 2024 alipo kutana na wananchi wa eneo hilo kusikiliza kero yao
"Nimekuja kuwasikiliza, pesa inatafutwa na Serikali na kila mtu atapata haki yake, na naomba leo iwe Siku ya mwisho kutoa elimu, ifike mahali tuelewane" amesema DC Mahawe na kuongeza;
Ndugu zangu hii ni Serikali haichezewi. Hakuna aliyejuu ya Sheria. Mlipewa vizuri elimu, watu wanaitisha vikao tumekuja kutoa elimu kwa mara ya mwisho. Ninyi sio pekeyenu mnadai fidia
hatutakubali kuinyima Wilaya amani" ameeleza
Kama pale tulijibiwa vizuri na Naibu Waziri. Tumeambiwa tuvute subira mpaka pale pesa zitakapo kuja
Iboya ikijengwa ni maendeleo ya ninyi wenyewe, tusifanye fujo. Hatutakaa tena kikao kingine wizara imeshapelekewa"
Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Songwe, Mhandisi Salvan H. Mloka amesema kuwa "Mradi huu upo na mpaka sasa kuna wataalamu wameshafika katika Wilaya yetu na mradi huu tutaanza kwa maana hiyo ni kitu ambacho kipo na fedha itakapopatikana mtaziona tu" amesisitiza
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, George Musyani ameeleza kuwa Wananchi wa Ihanda wana wajibu wa kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea mradi huo.
"Kupitia mradi huu wana Ihada wana wajibu kumshukuru usiku na mchana Mheshimiwa Rais sasa mivutano hii inakuwa sio sawa. Mradi huu utachochea ukuaji wa Wilaya na ukuaji wa maendeleo kwa ujumla. Wana Ihanda kuweni wa moja, na inapokuja miradi ndo maendeleo yanakuja, na mradi huu utakuzabpato la halmashauri" ameeleza mwenyekiti huyo na kuongeza;
"Tufuate itifaki za uongozi kama una kero tushirikishane kwa kufuata utaratibu , tuna kiu sana na mradi huu
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa