Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Ester Mahawe amemuomba Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kuwajengea hospitali ya Wilaya badala ya kurekebisha hospitali ya Wilaya ya Vwawa iliopo sasa.
DC Mahawe ametoa ombi hilo leo Jumatano Septemba 13, 2023 wakati wa ziara ya siku tatu ya Waziri Ummy katika Mkoa Songwe.
Amesema kuwa miundombinu ya hospitali ya Wilaya ya Vwawa ni chakavu na ilijengwa muundo wa zaman hivyo ukarabati utagharimu fedha nyingi kuliko kufanya ujenzi upya.
"Mhemiwa Waziri miundombinu ya hospitali hii ya Wilaya ilijengwa kama kituo cha afya cha zamani na mpaka utanuzi wake lilikuwa linaongezwa jengo moja moja mpaka yamefikia haya"
"Pia nafasi imejaa hakuna eneo la kufanya utanizi katika eneo hili , hivyo tunaomba kujengewa hospitali itakayo kuwa ya kisasa ili huduma iendane na majengo" ameomba DC Mahawe
Akizungumza katika ziara hiyo Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu amesema kuwa amepokea ombi hilo la DC Mahawe akiwaagiza waandike barua kwa TAMISEMI ili wapate kuwataarifu juu ya ombi hilo.
Waziri huyo amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan hana deni na watanzania kwasababu kila mwezi anatoa fedha za kununulia dawa
Waziri Ummy amewaagiza wanaohusika katika kiagiza dawa waagize dawa kwa wakati na kufanya makadirio ya dawa yalio sahihi Ili wananchi wapate huduma bora katika vituo vya kutolea huduma za afya
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa