DC MAHAWE AKUTANA NA WATUMISHI WA AFYA WILAYA YA MBOZI
Kutokana na kuwepo wa malalamiko ya wananchi katika maeneo mbalimbali kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya, Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mhe. Esther Mahawe amelazimika kukutana na watumishi hao ili kutafuta ufumbuzi wa kero hiyo.
Kikao hicho kilichohusisha timu ya usimamizi huduma ya afya, waganga wafawidhi wa hospitali, vituo vya afya na zahanati na watumishi wa hospitali kimefanyika leo Ijumaa Februari 9, 2024.
Akizungumza katika kikao hicho Mkuu Wilaya hiyo amesema kuwa kutokana na 'hiracky' ya hospitali iliyopangwa vizuri sio kwa bahati mbaya kila mmoja akianza kutengeneza vizuri eneo lake hakutakuwa na kero kwa wananchi
"Mpaka malalamiko yanatoka huko mpaka kwa viongozi wakubwa kama kero zilizoibuka juzi kwa mkuu wa Mkoa mnakuwa na lugha mbaya na za karaha kutoka kwa wauguzi hasa wanaofanya kazi katika chumba cha kujifungulia, mbaya zaidi wahudumu wanawake
Hakuna mwanamke asiyejua mapito ya mwanamke anayejifungua anayopitia kipindi cha kujifungua, japo sio wote wenye kauli mbaya" amesema na kuongeza;
Kwanini mnashindwa kuwa na lugha nzuri za kumfariji mtu?" Amehoji Mkuu huyo wa Wilaya
Sambamba na hilo, Amehimiza watumishi wote wa afya kuhakikisha wanavaa vitambulisho ili kuwaatambua kwa majina wanapohudumia wagonjwaMISHI WA AFYA WILAYA YA MBOZI
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa