MBOZI. Mkuu wa Wilaya ya Mbozi (DC), Esther Mahawe amekutana na kufanya mazungumzo viongozi wa dini katika wilaya hiyo kujadili mustakabali wa wilaya hiyo.
Kikao hicho kimefanyika leo Jumatatu Februari 2023 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi
Katika kikao hicho mkuu wa wilaya huyo amesema kuwa amekutana na viongozi hao ili kujua maono yao juu ya wilaya hiyo.
"Nimekutana na nyie kikundi cha kwanza ni viongozi wa dini kikao cha kufahamiana na nilikua napenda kuanza na Mungu katika wilaya yetu,
Nimekutana na ninyi ili kujua maono yetu ya wilaya ya Mbozi. Tunazaidi ya watu laki tano nikasema nisipokaa nanyi nikajua mapokeo yenu, nikajua njozi zenu huenda nikakosa ushirikiano nilioutarajia" amesema mkuu huyo wa wilaya.
"Binafsi naamini katika ushiriki kwamba wewe kama kiongozi wa dini ukibeba sehemu ya jukumu lako la kuiombea wilaya yetu haitapata shida"
Ametoa rai kwa viongozi hao kuwakumbusha waumini kusimaia malezi.
"Turudi kwenye malezi tuwakumbushe waumini wetu, watoto wetu na vijana wanacheza kamari na pia tuangalie tunavyoishauri jamii ili kuepusha masuala ya visasi na taharuki"
Amesisitiza kuwa "Naomba turudi katika maadili yetu watu wasijifiche kwenye mwamvuli wa dini tutachukua hatua kama wahalifu wengine"
"Ulinzi usipotoka kwa Mungu ni kazi bure, natamani kuona tunashirikiana kwa ukaribu, binafsi napenda uongozi unaoacha alama watu wakukumbuke Kwa ulichofanya" amesema
Mkuu wa Wilaya huyo amesema kuwa yeye ni mfaatiliaji na atatumia muda mwingi kwenda kufuatilia miradi na kisikiliza kero za wananchi huko vijijini.
Katika masuala ya utekelezaji wa miradi DC huyo amemtaka mkurugenzi kuwakumbusha watumishi kuwa hatapokea mradi mbovu kwasababu yenye ni mtu anayesimamia katika viwango
"Mkurugenzi uwaambie kabisa watumishi sitapokea mradi mbovu, Mimi ni injinia nisie na cheti sitakubali mradi mbovu" amesisitiza
Aidha DC huyo ametumia kikao hicho kupiga marufuku kuwatoza fedha akinamama wajawazito wanaotozwa fedha kipindi wanachokwenda kujifungua katika hospitali za serikali.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa