MBOZI. Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Ester Mahawe amesema kuwa wanawake wajawazito wanaofika kujifungua katika vituo vya afya vya Serikali Wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe, hawatakiwi kutozwa fedha.
Amesema hayo kwenye kikao cha machifu na wazee maarufu alichoitisha kwa lengo la kufahamiana na kujadili mwendelezo wa maendeleo waliyofanya watangulizi.
Mkuu huyo wa wilaya amesema ametoa maekekezo kwa Mkurugenzi kuwa wanawake wajawazito wanapofika kujifungua kwenye vituo vya afya vya Serikali hawatakiwi kutozwa fedha yoyote.
Pia ameongeza kuwa wazee na watoto chini ya umri wa miaka mitano nao watatibiwa bure na kuwa suala hilo atalisimamia kwa ukaribu zaidi ili huduma hizo zitolewe kama maekekezo yalivyotolewa.
Kaimu Mkurugeni wa Wilaya ya Mbozi, Danny Tweve amesema wazee wanatakiwa kufika kwa watendaji wa maeneo yao ili kupewa utaratibu jinsi ya kupata vitambulisho ili kurahisisha utambulisho wao.
Baadhi ya wazee maarufu waliohudhuria kikao hicho, Wilihadi Njeje amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Mbozi kwa mwanzo mzuri wa kushirikisha makundi maalumu na kwamba ni ishara nzuri na kuwa viongozi waliofanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo ni pamoja na kuwashirikisha wananchi wake.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa