Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbozi, ndugu Mbwana Kambangwa amewataka wataalamu wa tiba asili kufuata taratibu zinazoongoza huduma zao huku akikemea wanaofanya ramli chonganishi.
Kambangwa ametoa rai hiyo leo Jumamosi Aprili 20, 2024 wakati akiongea na wataalamu hao wa tiba asili huku akiwataka wale wanaotoa huduma hili bila kujisajili wafute taratibu za kujisajili.
"Pamoja na kutambuliwa na Serikali nanyi mna changamoto wengi wenu hamjajisajili Ili mtambuliwe. Inatakiwa muwe na leseni na chama chenu mjisajili. Mnatakiwa kujitambua kama wewe ni mtaalamu kwanini usijisajili" amehoji
Amewataka wale wanaofanya ramli chonganishi kuacha tabia hiyo kwa kuwa ina madhara makubwa.
"Mnachangamoto ya kufanya ramli chonganishi ambayo inamadhara makubwa ktk jamii. Watu wanashindwa hata kuzikana, hii lamli chonganishi inatupelekea kuto kuaminika, zinagombanisha na kuharibu tiba asili. Tutaharibu soko letu, leo umemchanganisha mtu kesho atakuja?"
Ameeleza kuwa kutokana na ramli chonganishi zinasabsbisha baadhi ya watu kufanya mauaji. Unaenda kumchinja mtu anategemewa na familia, ili uwe na mali lazima ufanye kazi kwa bidii, hii inaharibu heshima yetu"
"Kweli tunatafuta fedha. Ukipata mali kwa njia haramu haina baraka kwasababu fedha Ile ni haramu unapata majanga mengi na hazidumu, au zinakuwa chanzo Cha maafa kwa ndugu zake" amesisitiza na kuongeza;
"Wengine tunaendesha hapa huduma za ukunga ukiona kuna changamoto muwahishe hospitali kuokoa uhai wake. Huwezi kufanya oparesheni, unakaa na mgonjwa pale umekaa unakula fedha ya ile familia laana lazima ikupate, damu zao lazima zirudi kwenye kizazi chako" amesema
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa