• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI WA VWAWA-MLOWO WATAKIWA KULIPA BILI ZA MAJI KWA WAKATI

Kurushwa hewani: August 17th, 2023

Wananchi wa mji wa Vwawa na Mlowo wilayani Mbozi wametakiwa kutoa maoni yatakayosaidia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Vwawa-Mlowo (WSSA)  kutoa huduma bora ya maji.

Pia, wametakiwa kulipia bili za huduma ya maji kwa wakati na kuhifadhi miundombinu ya maji katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa leo Alhamisi Agosti 17, 2023 na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Esther Mahawe akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dk Francis Michael wakati akifungua mkutano wa taftishi kuhusu ombi la kurekebisha bei za huduma za maji safi na usafi wa mazingira za Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Vwawa-Mlowo (WSSA) uliondaliwa na Ewura unaoendelea mjini Vwawa.

DC Mahawe amesema "Wananchi wana haki ya kutoa maoni ya huduma wanayoipata na wana haki ya kupata huduma kwa wakati na ubora hivyo nawaomba mtoe maoni yatakayosaidia mamlaka kutoa huduma bora na changamoto mnazokutana nazo"

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Mhandisi Mkuu Violet Iram amesema kuwa mapendekezo ya marekebisho hayo yaliyopendekekezwa na WSSA yanalenga kuiwezesha Mamlaka kutekeleza shughuli zilizoainisha katika mpango biashara wake kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2023/24 na 2025/26.

"Bei zinazopendekezwa zitasaidia shirika kurejesha gharama za uendeshaji na matengenezo pamoja na kukidhi baadhi ya gharama za ukarabati, uingizwaji na uwekeaji mpya na hivyo kutoa huduma ya maji ya kutosha, safi na salama katika maeneo ya huduma Vwawa-Mlowo" amebainisha

Mkurugenzi Mtendaji wa WSSA, Mhandisi Clavery Casmir amesema kuwa mabadiliko hayo ya bei za maji yatawasaidia kukamilisha miradi mbalimbali inayotekelezwa ili kuboresha usambazaji wa maji kwa wananchi wa Vwawa na Mlowo.

Amesema Mamlaka hiyo pia ina mkakati wa kutoa maji mto Momba ambapo mradi huo utasaidia kutatua adha ya maji kwa mji wa Tunduma, Vwawa na Mlowo.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa