• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

SHULE YA WENYE MAHITAJI MAALUMU WAISHUKURU SERIKALI, WATOA MAPENDEKEZO, MBOZI

Kurushwa hewani: March 21st, 2023

Mbozi. Uongozi wa Shule ya Msingi Mwenge kitengo Cha wanafunzi wenye mahitaji maalumu iliyopo wilayani Mbozi  umeishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuwepo  wanafunzi wenye ulemavu na kuwapa fursa ya kupata elimu.


Shukrani hizo zimetolewa leo Jumanne Machi 21, 2023 wakati wa ziara ya wakuu wa idara wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi (CMT) katika shule hiyo.


Akisoma taarifa ya kitengo hicho mwalimu wa wanafunzi wasioona,  Revina Kayombo amesema kuwa wanaishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kwa kuwapelekea kitengo cha iposa kwa wanafunzi wenye ulemavu wa akili ambacho kitengo hicho kinawasaidia kujifunza masuala ya ufundi baada ya kumaliza elimu ya msingi kama hawajachaguliwa kujiunga na sekondari.


"Wanafunzi hawa wanaweza sana masuala ya ufundi na michezo na wanaweza kufanya vizuri zaidi"


Mwalimu huyo ametaja changamoto wanazokutana nazo katika kitengo hicho ikiwemo ukosefu wa kisima cha maji ya kudumu, choo maalumu kwa wanafunzi wenye ulemavu wa viungo, uzio wa bweni la kike.


Changamoto zingine alizozitaja mwalimu Kayombo ni pamoja na uhaba wa vyumba vya madarasa, bwalo la chakula, vifaa vya kufundishia na kujifunzia, upungufu wa walimu, vifaa vya michezo, maktaba, samani na uwanja wa michezo.


Uongozi huo umetoa  mapendekezo ya kuwepo matangazo maalumu kuhusu watu waenye mahitaji maalumu ili kuwafikia kwa urahisi.


Pia, umeomba  mazingira ya shule kuboreshwa kulingana na mahitaji ya watoto wenye ulemavu, serikali kuajiri mlinzi, mpishi na matroni wenye uelewa na elimu maalumu.


Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha elimu maalumu shuleni hapo, Eden Ngogo ametaja mchakato wa kuwapata watoto hao kuwa ni pamoja na kuzunguka majumbani kuwatafuta, kutoa elimu katika nyumba za ibada, kupata taarifa kutoka kwa watu mbalimbali.


Mkuu huyo ambaye pia ni mlemavu wa macho ameiomba Serikali kuanzisha sekondari ya mkoa ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu ili kuzidi kuwasaidia watoto hao kuyafikia malengo yao.


Mwalimu wa wanafunzi wenye ulemavu wa akili, Alois Chacha amesema kuwa kuna watoto ambao wanamatatizo ya akili lakini wanamudu suala la michezo.


Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Oscar Mgani   amewapongeza walimu wa shule hiyo hasa kitengo cha elimu maalumu kwa kuwafundisha na kuwahudumia wanafunzi hao.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI MBOZI DC May 23, 2023
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • *WAFANYAKAZI WAIPA TANO SERIKALI, WAOMBA KUBORESHEWA MISHAHARA, SONGWE

    May 02, 2023
  • RPC ATAKA USHIRIKIANO KUTOKOMEZA UKATILI, SONGWE

    May 02, 2023
  • MADIWANI WAMPONGEZA MKURUGENZI WA HALAMASHAURI KWA UNUNUZI WA EXCAVATOR, MBOZI

    May 02, 2023
  • MADIWANI WATAKA WANAOFANYA UKATILI WACHUKULIWE HATUA, MBOZI

    May 02, 2023
  • Ona vyote

Video

video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa