Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt Fransis Michael ametaja vipaumbele vinne huku akiwaomba watumishi wa umma katika mkoa huo kuungana.
Dkt Michael aliteuliwa Jumapili Februari 26, 2023 kuchukua nafasi ya Waziri Kindamba ambaye alihamishiwa Mkoa wa Tanga.
Akizungumza wakati akikabidhiwa ofisi rasmi na aliyekuwa mkuu wa mkoa huo leo Jumatatu Machi 20, 2023 Dk Michael amesema kuwa kipaumbele chake cha kwanza ni ulinzi na usalama kwa wananchi na mali zao.
"Kipaombele changu cha kwanza nu ulinzi na usalama wa raia na mali zao, nitahakikisha vinatiliwa mkazo na nashukuru sana kwa kuwa kamati ya uliznzi na usalama mkoa wananipa ushirikiano" amesema
Amewataka wananchi kuhusika katika suala la ulinzi bila kuviachia vyombo vinavyohusika pekee.
Kipaumbele cha pili alichotaja mkuu huyo wa mkoa ni usimamizi wa miradi ya maendeleo.
Amesema kuwa miradi ya maendele inayotekelezwa na Serikali ni fedha za wananchi na walipa kodi hivyo amewaagiza wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri za mkoa huo kusimamia na miradi hiyo.
"Nitakuwa mkali kwa hili, kwa miradi ambayo tunatakiwa tuisimamie tukaisimamia viuri,
Tunapaswa kuhakikisha miradi ya maendeleo na fedha tunazokusanya zinatumika ipasavyo.
Kipaombele cha tatu cha mkuu huyo wa mkoa mpya ni utoaji wa mikopo ya alilimia 10 kutoka kwa hamlamshauri kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.
"Wenyeviti wa halmashauri simamieni hili suala ili wanaopaswa kupata hizi fedha wapate".
Mkuu huyo wa mkoa ametaja jambo lingine ambalo atalisimamia kuwa ni utunzaji wa mazingira.
"Utunzaji wa mazingira ni jambo la msingi na wote inatakiwa tulitilie mkazo" amesema
Dk Michael ametaja jambo lingine atakalozingatia katika uongozi wake kuwa ni ushirikiano kwa watumishi na taasisi mbalimbali ili kuweza kuupaisha Mkoa wa Songwe.
"La mwisho ni ushirikiano, nitawaomba ushirikiano wa hali ya juu sana. ushirikiano ni jambo la msingi sana" amesema Dk Michael akitaja vipaumbele huku akimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumuamini na kumteua katika nafasi hiyo.
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe (RAS), Happiness Seneda amesema kwa niaba ya viongozi na watumishi wa umma wa mkoa huo wamepokea maelekezo na anaamini kila mtumishi atayatekeleza.
"Tumepokea maelekezo na kila mmoja amesikia.Tutakusikiliza na tutakupa ushirikiano ili kutimiza azma ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwatumikia wananchi ikamilike" amesema
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa