• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

KIGAHE: TRA WAFUATENI WAFANYABIAASHARA

Kurushwa hewani: August 10th, 2023

 Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe amewataka watumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Songwe kuwafwata wafanyabiashara katika maeneo yao ili kuwapa elimu na kujadiliana namna ya kulipa kodi badala ya kuwasubiria wafanyabiashara kuja ofisini.

Kigahe ameyoa agizo hilo leo Jumatano Agosti 10, 2023 wakati wa mkutano wake na  baadhi ya  wafanyabiashara wa mkoani huo mjini Vwawa.

"Mimi nadhani muende katika maeneo yao ya biashara badala ya kuwasubiri wafanyabiashara kuja ofisini" amesema na kuongeza;

"Tutoke tukawaelimishe watu. Naona mkienda katika maeneo ya wafanyabiashara mtatoa elimu na kukubaliana namna ya kupanga kodi na utaratibu huo utakuwa na matokeo chanya" amesema

Akizungumza katika mkutano huo Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Songwe, Aderick Alphonce  amesema kuwa wamepokea maagizo hayo na wanakwenda kuyafanyia kazi.

"Kuanzia sasa tutakuwa tunakuja katika biashara zenu kutoa elimu na msiwaogope maofisa wa TRA" ameahidi Kaimu Meneja huyo wa TRA.

Akizungumzia kuhusu changamoto ya Barabara ya Tanzam, Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbozi (DAS), Mbwana Kambangwa amesema kuwa barabara hiyo imeanza ujenzi wake ambapo ikikamilika itatatua changamoto ya usafirishaji.

"Changamoto ya barabara kutoka Igawa mkoa wa Mbeya mpaka Tunduma mkoa wa Songwe inajengwa kwa thamani ya Sh1.1 trilioni na itajengwa kwa kiwango cha kimataifa. Tunamshukuru sana Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha hili" amesema Katibu Tawala huyo.

Baadhi ya wafanyabiashara wameiomba Serikali kupitia halmashauri kupunguza kodi na tozo mbalimbali ili kuwafanya wafanyabiashara hao kulipa kodi.

Pia, wameiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoa elimu ya mlipa kodi pamoja na kujenga urafiki na wafanyabiashara hao.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga Mkoa wa Songwe, Kelvin Kyando amesema kuwa kumekuwa na kodi zisizo na usawa ambazo zinawakimbiza wafanyabiashara wengi.

"TRA wawe na tabia ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara waweze kulipa kodi kwa urahisi. Pia watengeneze mazingira rafiki kwa wafanyabiashara" amesema Kyando

Naye mfanyabiashara Georgina Chaula ameiomba Halmashauri kupunguza kodi kwa wafanyabiashara wadogo.

Kwa upande wake mfanyabiashara wa mchele amesema kuwa hakuna soko maalumu la mchele katika mji wa Vwawa pamoja na pumba hivyo kuomba kutengewe eneo maalumu.

Naibu Waziri Kigahe yupo kwenye ziara ya siku mbili katika Mkoa wa Songwe ambapo jana alitembelea Kituo cha Pamoja cha Forodha cha Mpaka Tunduma katika mpaka wa Tanzania na Zambia

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa