• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

KAMATI YATOA SIKU 14 UKAMILISHAJI ZAHANATI YA SHILANGA, MBOZI

Kurushwa hewani: April 6th, 2023

MBOZI. Kamati ya Uchumi, Fedha na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imetoa wiki mbili kwa kijiji cha Shilanga kata ya Ihanda kupiga hatua ukamilishaji wa zahanati ya ya kijiji hicho baada ya kupokea Sh50 milioni kwaajili ya ukamilishaji  lakini bado hawajaanza kuzifanyia kazi.


Agizo hilo limetolewa leo Jumatatu Aprili 3, 2023 na Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mbozi, George Musyani wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika halmashauri hiyo.


Musyani amesema kuwa kijiji kilishapokea Sh50 milioni tangu mwezi Februari mwaka huu lakini mpaka sasa hakijaanza ujenzi.


Amesema kuwa kama wiki mbili zitapita bila utekelezaji wa agizo hilo, fedha hizo zitahamishiwa kwenye vijiji vingine ambavyo vina uhitaji.


"Baada ya sisi kuondoka mkae kama kijiji mjadili jinsi gani mtakamilisha kazi hii, baada ya wiki mbili tutakuja kukagua kuwa mmefikia wapi na kama bado mtakuwa mnasuasua fedha hizo tutazihamisha na kuzipeleka katika vijiji vinavyohitaji" amesisitiza mwenyekiti huyo wa halmashauri.


Amesema " Kila kitu mnacho, fedha mnazo sio kusema kuwa kuna kitu mnakitafuta ni mchakato tu unasuasua kuanza, kwa kusuasua huku inaonyesha nyie hamna uhitaji"


Mwenyekiti huyo amesema kuwa ameshangazwa na taarifa za kuwa wananchi hawahudhurii kwenye mikutano ya kijiji kutokana na kokosekana kwa posho.


Kwa upande wake Diwani wa Viti Maalum Tarafa ya Vwawa, Neema Nzowa amewataka wananchi wa kijiji hicho kuhudhuria mikutano ya kijiji ili kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Diwani huyo amesema kuwa inawezekana wananchi hawahudhurii mikutano ya vijiji kutokana na kusitishwa kwa posho zilizokuwa zikitolewa kipindi cha nyuma.


Mkazi wa kijiji hicho, Adam Senka amewataka wananchi kuwa wafuailiaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili itekelezwe kwa wakati.


Ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itawahuumia wananchi zaidi ya 400 ulianza mwaka 2011.


Kwa sasa wananchi wa kijiji hicho wanalazimika kwenda katika Zahanati ya Ihanda au Hospitali ya Wilaya ya Mbozi kupata huduma za afya.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa