• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

DC MBEGA AONGOZA ZIARA YA KAMATI YA FEDHA YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBOZI KUJIFUNZA MBINU BORA ZA UKUSANYAJI WA MAPATO TEMEKE

Kurushwa hewani: February 24th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. Hamad Mbega ameongoza Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi pamoja na baadhi ya Wakuu wa Idara za Halmashauri ya Wilaya hiyo katika ziara maalumu katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke kwa lengo la kujifunza mbinu bora za kuongeza ukusanyaji wa mapato pasipokutegemea mazao ya kilimo.


Ziara hiyo imefanyika leo Jumatatu Februari 24, 2025 ambayo imelenga kuboresha utendaji wa Halmashauri kwa kuiga mifano bora ya usimamizi wa ukusanyaji wa mapato.


Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imekuwa na mafanikio katika usimamizi na ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mifumo ya kidijitali na mbinu za kisasa hasa kuanzishwa kwa Cluster (kanda 06 za ukusanyaji wa mapato).


Katika ziara hiyo, Kamati hiyo ilipata fursa ya kujifunza namna ya kuimarisha vyanzo vya mapato vinavyotokana na sekta zisizo za kilimo kama leseni za biashara, vibali vya ujenzi, service levy n.k


 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Temeke Mhe. Abdallah Mtinika amesema kuwa Manispaa hiyo ndio inaongoza kwa ukusanyaji wa mapato Mkoa wa Dar es salaam ambapo mwaka 2023/2024 walikusanya mapato ya ndani kwa asilimia 100 na kwa mwaka wa fedha 2024/2025 hadi kufikia Disemba, 2024 Manispaa ilikuwa imekusanya mapato yake ya ndani kwa asilimia 58.


Mstahiki Meya aliongeza kuwa katika Mwaka wa fedha 2025/2026 Manispaa imejiwekea lengo la kukusanya Tshs 63 Bilioni.


Katika kikao hicho Meya huyo alibainisha kuwa Manisipaa ya Temeke ilivyofanikiwa kuongeza mapato kwa asilimia 30 kupitia uboreshaji wa mfumo bora wa ukusanyaji pamoja na kuongeza nguvu kazi ya wakusanyaji mapato na vyombo vya usafiri vinavyowafanya kupenya kila mahali kwaajili ya kufutilia mapato.


Aidha katika ziara hiyo Kamati ilifanikiwa kutembelea maeneo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Mbagala Rangitatu na Klasta ya ukusanyaji wa mapato Charambe na kujionea jinsi mapato yanavyokusanywa moja kwa moja bila mianya ya upotevu wa fedha

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa