Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mhe. Esther Mahawe amewataka wananchi Wilaya hiyo kujenga nyumba zao kwa kuzingatia kanuni bora za ujenzi Ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kipindi cha mvua na upepo mkali.
Mkuu wa Wilaya huyo ameyasema hayo Jumanne Disemba 11, 2023 wakati akikabidhi msaada kwa waathirika ambao nyumba zao zimebomolewa kwa upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa.
DC Mahawe amesema kuwa asilimia kubwa za nyumba za Wilaya hiyo za vijijini zimejengwa bila kufungwa lenta ambayo inasababisha nyumba hizo zisiwe imara.
"Jamani Wanambozi wenzangu nyumba nyingi tunazojenga huku vijijini hazina lenta na mwenyekiti hapa amenidokeza zinajengwa kwa siku tatu mpaka nne kitu ambacho sio sawa haziwezi kuwa imara"
"Pia katika maeneo yetu tumekata miti mno, sasa upepo ukija kunakuwa hakuna kitu cha kuzuia unaenda moja kwa moja kwenye nyumba unaharibu"
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi akiwa na kamati ya maafa ya Wilaya ya Mbozi na kamati ya usalama Wilaya wamekabidi vitu mbalimbali kama msaada katika familia zilizo athirika zaidi vitu vyenye thamani ya shilingi milioni 9,030,000
Familia hizo zimepewa mabati 11 Kila kaya,misumari ya bati kilo 2, mifuko ya saruji, godoro moja kaya na madebe 2 ya mahindi kila kaya
Hata hivyo nyumba zilizoathirika na mvua hizo ni nyumba 171 lakini kipaumbele katika kugawa msaada huo imezingatia watu wenye mahitaji maalum, wajane, watu wenye hali duni na pia nyumba zilizobomoka kabisa.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa