• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Mbozi District Council
Mbozi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango , Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Idara ya Maji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Idara ya Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Maliasili
    • Vitengo
      • Wakaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha, Mipango na Uongozi
      • Kamati ya Uchumi
      • Kamati ya Elimu, Afya na Maji
      • Kamati ya Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao
    • Ratiba ya kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
      • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
    • Majarida Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi au kitaifa
    • Hotuba za viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio

SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

Kurushwa hewani: December 1st, 2020

SONGWE: WANANCHI WAHIMIZWA KUPIMA UKIMWI KUJUA HALI ZAO KUEPUKA MAAMBUKIZI MAPYA

Wananchi wa Mkoa wa Songwe wahimizwa kupima UKIMWI kujua hali zao za maambukizi hii inatokana na Mkoa kuwa na 86% ya watu wanaoishi na UKIMWI kufahamu hali zao wakati lengo la kitaifa tunatakiwa kufika 90% au zaidi watu kujua hali zao za maambukizi kwa wanaoishi na UKIMWI.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Breg. Jen. Nicodemus Mwangela amewataka watalamu wa Afya ifikapo Desemba 2021 kuhakikisha Mkoa uwe umetimiza lengo la 90% kwa kuwafikia wananchi wote ambao wanapaswa kujua hali zao za maambukizi ya UKIMWI.

Mkuu wa Mkoa ametoa agizo ilo katika maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani ambayo ufanyika kila Desemba mosi nas kwa Mkoa yamefanyika Wilaya ya Mbozi eneo la Ivungwa-Karasha na Hotuba ya Mkuu wa Mkoa kusomwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Mhe. John Palingo.

“Kwa kutofanya vizuri katika 90 ya kwanza kutapelekea watu wanaoishi na UKIMWI kutotambua hali zao hali ambayo itapelekea kuongezeka kwa maambukizi mapya katika jamii na kupunguza kasi ya kupambana na UKIMWI, kwani msimamo wa Mkoa wa Songwe ni kuwa Mkoa wa kwanza ifikapo 2030 kwa kumaliza kabisa maambukizi mapya ya UKIMWI, vifo vitokanavyo na UKIMWI na kutokomeza ubaguzi kwa walioathirika na UKIMWI huu utakuwa mchango wetu mkubwa kwa Tanzania” Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Breg. Jen. Nicodemus Mwangela.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dr. Hemed Nyembea amesema mikakati ya 90 tatu za kupambana na UKIMWI Songwe tunafanya vizuri kwenye 90 ya pili na tatu tub ado nguvu inatakiwa katika 90 ya kwanza, 90 ya kwanza watu wote wanaoishi na UKIMWI waweze kupima na kutambua hali zao, 90 ya pili wote waliopata UKIMWI kuanzishiwa dawa za kufubaza kwa 90 ya pili tumefika 96% na kwa 90 ya tatu inataka wote wanaoishi na UKIWMI wanaendelea kupata Dawa Songwe tumefika 95%.

Dr. Nyembea amesema Mkoa unaendelea na mkakati wa kupamba na UKIMWI kwa kuendelea kutoa ya huduma ya kupima kwa wananchi kwa kulengwa wale wenye sifa, kujikita kubaini watu wote wenye sifa ya kupimwa UKIMWI wanapokuja kwenye vituo vya kutolea Huduma pamoja na kuendeleza mkakati wa kufika lengo la 90 ya kwanza.

Mkazi wa Mbozi, Eliud Mwashambwa ameiomba Serikali kuendelea kuhamasisha watu wapime UKIMWI kupitia mikusanyiko mbalimbali inayokuwepo ili kuweza kutimiza lengo la 90% ya watu wanaoishi na UKIMWI kutambua hali zao.

Dr. Antony Galishi kutoka Worldvision Tanzania amesema shirika linaendelea kutoa elimu juu ya ukatili ya kijinsia na watoto katika makundi mbalimbali kwa kuwa ukatili nao umekuwa ni moja ya chanzo cha maambukizi mapya ya UKIMWI na lengo ni kuhakikisha ifikapo 2030 hakuna maambukizi mapya.

Mkoa wa Songwe una vituo vya Tiba ya Matunzo (CTC) 64 na vituo vya kukinga maabukizi ya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto 108.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA March 09, 2025
  • RASIMU PENDEKEZWA YA SHERIA NDOGO ZA MWAKA 2025. March 09, 2025
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • DC MBEGA AWATAKA VIONGOZI WA KATA KUSHIRIKIANA KATIKA UTENDAJI

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AGAWA SARE ZA SHULE KWA WANAFUNZI 120 WANAOTOKA MAZINGIRA MAGUMU ISANGU

    March 21, 2025
  • DC MBEGA AFANYA ZIARA KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI, ASISITIZA USHIRIKIANO KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI

    March 19, 2025
  • DC MBEGA ASISITIZA UIMARISHAJI NA USIMAMIZI MZURI WA AMCOS MBOZI

    March 18, 2025
  • Ona vyote

Video

VIJANA MSITUMIE MIKOPO YA 10% KUBET MBOZI
video zaidi

Kurasa za Karibu

  • You Tube
  • Katiba

Tovuti Muhimu

  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

Watembeleaji wa kimataifa

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

writingMasterThesis

Eneo la ramani

Wasiliana nasi

    Mbozi

    Anuani: 3

    Simu: 025-2580272

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa