Serikali imetoa shilingi Milioni 46 kuboresha miundombinu ya Shule ya msingi Shititi iliyopo Kijiji cha Mpanda Kaya ya Nyimbili.Fedha hiyo inajenga miundombinu ya kisasa madarasa 2 na vyoo matundu 6.Timu ya Watalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi imefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi na imeagiza kasi ya ujenzi iongozeke kwa kuwa fedha zipo zote.Mwalimu Mkuu wa Shititi, Mwl. Enifa Sasenga ameishukuru Serikali ya awamu ya 5 kwa kuwapatia fedha za ujenzi wa madarasa ya kisasa ambayo yanajenga taswira nzuri ya Shule na Kitongoji. Kukamilika kwa madarasa haya kutasaidia wanafunzi kusoma katika mazingira bora shuleni.
Mbozi
Anuani: 3
Simu: 025-2580272
Simu ya kiganjani:
Barua pepe: ded@mbozidc.go.tz
Hati Miliki 2017 Halmashauri ya Wilaya-Mbozi. Haki zote zimehifadhiwa